Sikiliza Clouds FM Live station ya watu.

Saturday, April 10, 2010

Ni huzuni kubwa kwa wananchi wa poland

Nchi ya Poland leo imejikuta iko kwenye huzuni kubwa baada ya raisi wao Lech Kaczynski kupata ajali ya ndege.Yeye na Maria ambaye ni mke wake ambaye ni mchumi walikufa papo hapo baada ya ndege yao aina ya Tupolev-Tu 154 kuanguka wakati ikijaribu kutua uwanja wa ndege wa Smolensk,Russia.Lech ana ndugu yake mapacha wa kuzaliwa ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu wa poland.Miongoni waliokuwamo kwenye ndege ni maofisa wa polisi wa poland ambao nao pia hakuna alienusurika.Walikuwa wanaenda kwenye kumbukumbu ya miaka 70 ya mauaji ya Katyn.
Anyway Russia wanafikiri kuna mkono wa mtu hapo manake Raisi wa Russia Medvedev ameamuru uchunguzi wa ajali ufanyike mara moja,na wanaoshugulikia uchunguzi huo ni tume ambayo inaongozwa na waziri mkuu wa Russia Vladimir Putin. Wahenga wanasema tusubiri tuone!!!!

No comments:

Post a Comment